tulipo. Tunakoelekea. 6. Tafakuri ya kila wiki. Kwa mtawala wa africa tulinayo/Kutoka kiongozi wa afrika tutamaniyo

04/08/2024

Kwa Mhe wa Africa tuliyonayo

Bomoa bomoa, bomoa makazi ya wanyonge. 

Tumia tumia, tumia dhana ya eti utawala wa sheria. 

Pora, Pora, pora ardhi ya walalahoi. 

Kwani nani wa kusema sheria zilizopo haitendi haki?

Usijali, usiwe na unyonge

Shikilia kamba ya maendeleo. 

Nani mwenye ujasiri wa kuuliza

Maendeleo ya nani?

Tenda kwanza

Halalisha baadai. 

Una wabobebezi lukuki

Watatafuta msamiati halilishi wa kisheria. 

Nani mwenye ubabe wa kuwapinga?

Ujiridhishe tu unawafanyiya mema wananchi wako

Upate wema duniani na aherani. 

Nani ya kujua au kujali

Kitakachotokea mbele ya safari?

Wasalaam

Niko nawe daima

Mwanasiasa chupukizi. 

***

Kutoka Kiongozi wa Afrika Tutamaniyo

Ondoeni picha zangu majumbani mwenu

Bomoeni sanamu zangu mitaani wenu.

Kwani mimi ni Mungu wa kuabudu?

Au Mrungu wa kubembelezwa?

Futeni jina langu vituoni

Wekeni majina ya mashujaa wetu

Akina Kinjikitile na Mirambo

Mzee Tambaza na Bibi Titi

Njoni tukaae pamoja

Muunganeni tupange pamoja

Kupambana na ubeberu wa Ulaya

Na ubabe wa Marekani. 

Karibuni tufichue vibaraka wao

Watawala vikaragosi.

Madalali wa rasilimali zetu

Wavurugaji wa urathi wetu. 

Wasalaam

Mtumishi wenu daima

Leave a comment

Hey!

I’m Bedrock. Discover the ultimate Minetest resource – your go-to guide for expert tutorials, stunning mods, and exclusive stories. Elevate your game with insider knowledge and tips from seasoned Minetest enthusiasts.

Join the club

Stay updated with our latest tips and other news by joining our newsletter.

Categories

Tags